BAADA YA KUNYIMWA PENZI,..MAMA AMNG’ATA ULIMI ‘SERENGETI BOY’
Alisema ilipofika saa 6:30 usiku wateja wengine wote waliondoka na kubakia mama huyo pekee, kitu kilichomfanya naye afunge baa. Lakini alipomaliza kufanya hivyo mama huyo alimfuata na kumweleza kuwa alihitaji kufanya naye mapenzi.
“Sikuwa na mazoea naye, nilipokataa kufanya naye mapenzi, alinisogelea na kunishika sehemu zangu za siri na kuanza kuzivuta, nilipopiga kelele akanishika kichwa na kunilazimisha ‘kunidendesha’, akafanikiwa kuingiza mdomo wake kwangu na kunikata ulimi wangu, akaondoka nao na kwenda kuutema karibu na mlango wa bar,” alisema Simon ambaye wahudumu wa hospitali hiyo wamelazimika kumwekea ndoo ili awe anatemea damu kutokana na kujaa mdomoni.
Alisema baada ya kukatwa ulimi ambao sasa unamletea maumivu makali, alifanikiwa kufika nyumbani kwake kabla ya tajiri yake kumchukua na kumpeleka hospitalini ambako amelazwa.
Jeshi la Polisi mkoani hapa limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa ameshatiwa mbaroni huku uchunguzi ukiwa unaendelea. Hali ya majeruhi inaendelea vizuri.
No comments:
Post a Comment